MSIMAMIZI
wa uchaguzi Kata ya Kagondo Sharifa
Mstafa, amnyima fomu mgombea udiwani wa Kata hiyo
aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Bukoba Anatory Amani,
kupitia tiketi ya chama cha (NCCR-MAGEUZI ) kwa madai ya kupokea
maelekezo kutoka kwa msimamizi wa Jimbo la Bukoba Mjini.
Mstafa,alisema
sababu ya kukataa kutoa fomu kumesababishwa na kupokea barua mbili kutoka chama
hicho moja ikitoka ofisi ya chama cha ( NCCR-MAGEUZI )Mkoa wa Kagera na
nyingine kutoka wilayani zikiwa na maelekezo tofauti.
Alisema
barua iliyotoka ofisi ya Mkoa ya chama hicho iliyoandikwa tarehe 18/08/2015
saa 9.58 Alasiri yenye kumbukumbu NA.NCCR-
MAGEUZI/MM/KU/VOL.11/14/03 iliyosainiwa na kamishna wa chama hicho
mkoa wa Kagera Peterson Mganyizi ikimtambulisha Anatory Amani kuwa
mteuliwa wa kugombea udiwani wa chama hicho na kuwa watampeleka kuchukua fomu
Agost 19 mwaka huu.
Aliongeza
kuwa Agosti 19 mwaka huu majira ya saa 2:3asubuhi alipokea barua kutoka
chama hicho ngazi ya Wilaya ikimueleza kuwa chama hicho hakina mgombea wa
udiwani Kata ya Kagondo.
No comments:
Post a Comment