Na
Juhudi Felix- KYERWA
Matukio
ya wananchi kujichukulia sheria
mikononi na kuwapiga,kuwachoma moto watuhumiwa wanaowakamata
yanazidi kuongezeka wilaya
ya Kyerwa na
Karagwe mkoani Kagera
baada ya wananchi wa Kitongoji
cha Nyabihara kijiji cha
Kibingo kata Kibingo
kupinga kisha kumchoma
kwa moto kijana
mmoja aliyetambuliwa kwa
jina la Thomas Tumuhirwe miaka (24) baada ya
yeye kumua mama
yake wa Kambo Juliana
Tumuhirwe miaka (57)
Akithibitisha
kutokea tukio hilo
jana afisa mtendaji wa kata ya
Kibingo Geofrey Mihambwe alisema tukio
hilo limetokea usiku wa Agosti 19 mwaka
huu ambapo kijana huyo ambaye kwa sasa ni
Marehemu alimuua Mama yake huyo kwa kumkata na panga sehemu ya shingo pia
kumchoma kisu kifuani juu ya
titi la kushoto.
Alisema kuwa
chanzo cha mauaji hayo kimetokana na visa vilivyokuwepo baina ya hao marehemu
na kuwa siku za nyuma kijana huyo
Thomasi Tumuhirwe aliwahi
kuhukumiwa kifungo jela kufuatia
kumuibia mama huyo mbuzi wake
watano.
Wananchi
walioongea na waandishi
wa habari katika
eneo la tukio
walisema kijana huyo
aliyeuwawa kisha kuchomwa moto
alikuwa akijihusisha na
vitendo vya wizi
wa mali kwenye
kijiji hicho.
Rutambi
Mabati alisema kuwa
kutokana na tabia
hizo wananchi ndiyo
maana waliamua kuchukua
hatua hiyo ili kukomesha
wizi na vitendo
vya kijana huyo.
Marehemu
mama Juliana Tumuhirwe miaka (57), hakubahatika kupata
mtoto katika maisha
yake kwani majirani walieleza
kuwa alikuwa akijufungua
watoto kisha wanafariki
dunia.
Polisi
wilayani Kyerwa limethibitisha kutokea kwa vifo hivyo ambapo mganga
mfawidhi kutoka zahanati ya Kibingo Diana Tamba alifika eneo la tukio na
kufanya uchunguzi wa kitababu kisha kuruhusu miili ya marehemu kuzikwa.
Hata hivyo polisi wamewataka wananchi kutojichukulia
sheria mkononi kuwa hakuna mwananchi
akiye juu ya sheria na kuwaasa kutii sheria bila shurti.
No comments:
Post a Comment