SHAHIDI wa nne kwa upande wa utetezi, katika kesi
ya aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Bukoba Anatory
Amani, amekamilisha kutoa ushahidi wake, baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa
wa Kagera kukubali kupokea CD mbili kama Vielelezo vya ushahidi wake.
Katika kesi hiyo ya Madai Namba mbili ya mwaka
2014, Amani anaiomba Mahakama hiyo imwamrishe
Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba, amfungulie
Ofisi na kumtimizia haki zake
kama Meya wa Manispaa hiyo.
Katika Vielelezo hivyo, Shahidi huyo ambaye ni
Afisa Habari wa mkoa wa Kagera, Silyvestar Raphael alitoa CD mbili moja na
Video na nyingine ya Sauti za mkutano ulioitishwa kwa ajili ya kusoma taarifa
za ukaguzi maalumu uliofanywa na CAG- katika manispaa ya Bukoba.
Agost 10 mwaka huu, shahidi huyo hakumaliza kutoa ushahidi
wake, baada ya kuibuka mabishano ya kisheria kati ya mawakili wa serikali wanaosimamia
kesi hiyo na Wakili wa malalamikaji Aron Kabunga juu ya kupokea au kutopokea Vielelezo
hiyo.
No comments:
Post a Comment