Friday, August 21, 2015

VIJANA WANAOJIITA VIBARU KATIKA MRADI WA REA WAGOMBA KUFANYA KAZI KISHA MALIPO YAO.


Na Juhudi   Felix-KARAGWE.

Vijana wanaofanya kazi katika mradi wa umeme vijijini (REA) katika  laini  ya Nkwenda wamegoma kufanya kazi kwa siku ya leo agosti 21 kisha kuzingira ofisi za Rea zilizopo Wilayani Karagwe kwa madai ya kutolipwa malipo yao kwa muda mrefu.

 Vijana hao ambao wameeleza kuwa shughuli yao ni kuchimba mashimbo na kutandaza nyaya za umeme wamefikia hatua hiyo baada ya kutolipwa malipo yao kwa muda wa wiki tano.

Wameeleza kuwa makubaliano ya kazi hiyo ni kulipwa kila baada ya wiki moja lakini makubaliano hayo yamevunjwa na kuwasababishia kuishi kwa kutangatanga kwani hawana pesa ya kujikimu.

Vijana hao wameeleza kuwa endapo ofisi za REA zitashindwa kuwapatia madai yao watahakikisha wanaharibu nguzo ambazo walikuwa wamekwisha kuzijenga kutokana na kuwa hawajatendewa haki zao za msingi.

Mhandisi wa REA wilayani Karagwe Baraka Marco amewataka vijana hao kuwa na subira na  muda wowote watalipwa madai yao ambayo wanadai kwani mipango ya kuwalipa pesa yao inaendelea.

No comments:

Post a Comment